Maaskari
wakiongoza msafara wa wanachuo ambao walikuwa wanaelekea kwa mkuu wa
mkoa
Maaskari
wakiwa kwenye ulinzi wakati wa maanadamano ya wanachuo waliokuwa
wanaelekekea kwa mkuu wa mkoa Dodoma
Wanachuo
wakiwa wameshika mabango ya kushinikiza ulinzi katika chuo cha St. John
Wanachuo
wa chuo kikuu wakiwa kwenye maandamano
Wanachuo
wakiwa kwenye maandamano kuelekea kwa mkuu wa mkoa hii ni kushinikiza
ulinzi kwa sababu ya matukio ambayo yanaendelea kutokea maana juzi
alifariki mwanachuo na usiku wa kuamkia leo wanachuo walivamiwa kwenye
chumbani baada ya kukata nindo ya dirisha na kuiba Laptop tatu na simu
tano na baada ya kuchukua vitu hivyo waliacha wamewafanyia vitendo
vibaya na pia waliachwa wamefungwa ili wasipige kelele.
Kwa hali
hii imesababisha maandamano ili kushinikiza ulinzi katika chuo cha St.
John kilichopo Dodoma mjini.
Wanafunzi hao ambao waliandamana umbali wa
kilomita tatu leo kutoka chuo kilipo
na kuishia viwanja vya Mwalimu Nyerere walidai wanalenga kufikisha
ujumbe kwa jamii kutambua vitendo vya kikatili vinavyofanyika chuoni
hapo.
Maandamano
hayo ambayo yalikuwa yakisindikizwa na
Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia,
yalipita katika mitaa mbalimbali ya
Manispaa ya Dodoma.
Waandamanaji hao ambao mbali na kuimba nyimbo
za kulilaumu Jeshi la Polisi kwa kushindwa
kuthibiti vitendo hivyo, pia mabango waliyokuwa wamebeba yalikuwa yakililaumu jeshi hilo.










