Ndugu wa marehemu Bhoke wameridhia hilo, hasa
baada ya mama yao pia kufariki kutokana na majeraha makubwa aliyopata
kutokana na kukatwa mapanga katika mgogoro huo.
Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji hicho, Johannes Masirori alisema kuwa familia hiyo imeondoka Desemba 28 usiku mwaka huu wakiongozana na mwili wa marehemu mama yao.
Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji hicho, Johannes Masirori alisema kuwa familia hiyo imeondoka Desemba 28 usiku mwaka huu wakiongozana na mwili wa marehemu mama yao.
“Wamebeba kila kitu… Wameahidi hawatarudi tena hapa maana yake wamehamia Kijiji cha Bunchanchari,” alisema.
Kuhusu mifugo waliyokuwa nayo wamekabidhi kwa
ndugu zao lakini mizigo ilipakiwa ndani ya gari lililobeba mwili wa
marehemu kwenda Bunchanchari.
Alisema hata familia ya mtuhumiwa iliyokuwa
inaishi karibu na marehemu Bhoke wamehama, kwa kuwa eneo hilo walikuwa
wanaishi kwa ajili ya kilimo na ufugaji na kuwa sasa wamehamia kwenye
mji wao ulioko Kitongoji cha Senta. Uchunguzi wa mwili wa Marehemu Bhoke
ulifanywa na mganga wa zahanati ya Maji moto, Thomas Wambura chini ya
usimamizi wa mkuu wa Kituo kidogo cha Polisi cha Majimoto koplo
Deogratias Paul, baada ya gari lililokuwa likimpeleka Inspekta Abdallah
Idd ambaye ni Mkuu wa Tarafa ya Ngoreme kuharibikia njiani.
Kwa mjibu wa Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji,
ng’ombe 35 na mbuzi 20 waliokuwa wameshikiliwa na ndugu wa marehemu
wamerejeshwa baada ya ndugu wa mtuhumiwa kulipa Sh160,000 kama gharama
za jeneza Sh100,000 na usafiri wa mwili wa marehemu Sh60,000.
Mtuhumiwa Masati mpaka sasa hajapatikana na inadaiwa ametokomea kusikojulikana.
MSINGI WA TATIZO
Ni mgogoro wa ardhi, ambao ulisababisha hadi wakafikishana baraza la ardhi wilaya, mtuhumiwa alishinda na Bhoke akakata rufaa baraza la ardhi la kata akashinda.
Ni mgogoro wa ardhi, ambao ulisababisha hadi wakafikishana baraza la ardhi wilaya, mtuhumiwa alishinda na Bhoke akakata rufaa baraza la ardhi la kata akashinda.
Mtuhumiwa alikata rufaa baraza la ardhi la wilaya
Musoma, ambako iliandikwa barua kuwataka watu hao kufika mahakama ya
Musoma januari 28,2013 kujadili jambo hilo.
Lakini Desemba 27,2012 wake wa mtuhumiwa
walikwenda kulima eneo hilo ambalo lina mgogoro, ndipo ugomvi ulipozuka
na kutokea mauaji hayo.
SOURCE:MWANANCHI
SOURCE:MWANANCHI