WANAFUNZI WALIONYIMWA KUVAA NGUO ZA KUBANA WAANDAMANA

Wanafunzi  wa kike wa Chuo Kikuu cha Ardhi (Aru), kilichopo jijini Dar es Salaam wameandamana mpaka ofisi ya serikali ya wanafunzi kupinga tangazo lililobandikwa chuoni hapo linalowataka kuanzia kesho wasivae nguo fupi na za kubana.
 
Tangazo hilo limebandikwa siku ya Alhamisi wiki iliyopita, majira ya saa 10 alasiri, likiwa na maandishi yanayosomeka: “kuanzia tarehe 1 mwezi wa kwanza hakuna mwanafunzi yeyote kuvaa nguo fupi na za kubana. Tunashukuru uongozi wa wanafunzi kutekeleza hilo kwani tulisikia katika vyuo vingine sasa zamu yetu.”
 
Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho, Matiko Chacha, amesema kuwa, baada ya wanafunzi kusoma tangazo hilo waliamua kufanya maandamano mpaka ofisi ya serikali ya wanafunzi ili kupata uhakika kama wana taarifa na tangazo hilo na kwa nini hawajashirikishwa.
 
Amesema kuwa, wao kama serikali ya wanafunzi hawakuwa na taarifa juu ya uwapo wa tangazo hilo. Hivyo, walishtushwa na ujio wao na kuwajibu kuwa hakuna kitu kama hicho hata kama lilikuwa labda ni agizo kutoka utawala lazima lingepita katika ofisi zao.

Wanafunzi hao walimwonyesha kiongozi huyo nakala ya tangazo hilo, ambalo halikuwa na jina wala saini ya mwandishi. 
 
Chacha ameongeza kuwa, amewatuliza wanafunzi hao na kufikia mwafaka baada ya kulichana tangazo hilo mbele yao na kuwahakikishia kutokuwapo kwa suala hilo na kuwa, hata kama lingekuwa ni la kweli, lazima lingepelekwa katika bunge la wanafunzi ili kufanyiwa maamuzi.
 
Amesema kuwa, ni vigumu kwa wanafunzi wa chuo hicho kuvaa nguo fupi kutokana na uhalisia wa masomo yaliyopo kumtengeneza mwanafunzi kuvaa mavazi ya staha, kama vile suruali.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo