RAIS JAKAYA KIKWETE KATIKA UFUNGUZI WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi Chuo cha UIinzi (National Defence College) leo Septemba 10, 2012 Kunduchi jijini Dar es salaam. Kulia kwake ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo hicho, Meja Jenerali Charles Makalala na kushoto kabisa ni aBalozi wa China nchini Tanzania Mhe. Lu Younqing. PICHA NA IKULU
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Mkuu wa Chuo cha UIinzi (National Defence College) Meja Jenerali Charles Makalala leo Septemba 10, 2012 baada ya kumkabidhi mfano wa funguo kama ishara ya kufungua rasmi chuo hicho kilichopo Kunduchi jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Chuo cha UIinzi (National Defence College) Meja Jenerali Charles Makalala baada ya kufungua rasmi chuo hicho kilichopo Kunduchi jijini Dar es salaam. Nyuma yao ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe Shamsi Vuai Nahodha anayefuatana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma hotuba yake kufungua rasmi Chuo cha UIinzi (National Defence College) kilichoko Kunduchi jijini Dar es salaam, pamoja na kuzindua kozi ya kwanza ya mwaka mmoja. Walioketi karibu yake ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Chuo hicho, Meja Jenerali Charles Makalala
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma akipozi na wanachuo wa kozi ya kwanza ya bmwaka mmoja katika Chuo cha UIinzi (National Defence College) alichofungua rasmi leo Septemba 10, 2012 Kunduchi jijini Dar es salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo