ELCT MAKETE YAZIDI KUWANOA WAELIMISHAJI WAKE


Mradi wa pamoja tuwalee wilayani Makete umewajengea  uwezo zaidi wawezeshaji  kutoka katika kata nane  za wilaya hiyo juu ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia unaojitokeza katika kata zao
      
Akitoa mafunzo hayo mwezeshaji wa haki za mtoto  na kinamama Bi Stela  Mdawa amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wawezeshaji hao kutoka katika kata nane za Makete ambazo ni  Bulongwa, Ipepo, Ipelele, Luwumbu, Iwawa, Isapulano na Iniho, na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo wataisaidia jamii kujikwamua na unyanyasaji wa kijinsia

Amesema unyanyasaji ama ukatili wowote ule ukiwemo wa kijinsia hupelekea madhara makubwa kwa jamii ikiwemo vifo ama maamukizi ya virusi vya Ukimwi hasa kwa wanawake ambao ndio waathirika zaidi wa vitendo hivyo, huku akiwataka washiriki kupeleka elimu waliyofundishwa katika kata zao

Kwa upande wao washiriki wa warsha hiyo wameonyesha kufurahishwa na mafunzo hayo na kuahidi kufikisha elimu hiyo kwa wanajamii pamoja na  kuunda klabu za watoto ili kusaidia kukomesha vitendo vya unyanyasaji vinavyofanywa na baadhi ya wanajamii hasa kwa kina mama na watoto
                      
Naye mratibu wa program ya Pamoja Tuwalee Mchungaji Ezekiel Sanga amesema mradi huo unafadhiliwa na watu wa Marekani  kupitia shirika la Africare kwa kushikiana na asasi ya ELCT Makete unatekelezwa kwa muda wa miaka mitano ijayo katika kata kumi za wilaya Makete kwa kushirikiana na dawati la unyanyasaji kutoka idara ya polisi kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii kuachana na vitendo vya unyanyasaji na ukatili
      
Na RIZIKI MANFRED


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo