WANANCHI WILAYANI MAKETE WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MAAMBUKIZI MAPYA YA VIRUSI VYA UKIMWI

Makete                                        

Wananchi wilayani Makete wametakiwa kujikinga na maambukizi mapya ya vvu kwa kuacha tabia hatarishi zinazopelekea mtu kupata ugonjwa wa UKIMWI

Hayo yamezungumzwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh, Daniel Okoka wakati akizindua kituo cha CTC katika zahanati ya kata ya Mfumbi nakusema lengo la kujengwa kwa kituo hicho ni kuweka huduma karibu na watu walio na maabukizi ya vvu

Katika uzinduzi huo pia Mh Okoka alikabidhi pikipiki aina ya bajaji katika zahanati hiyo ili iweze kubeba wagonjwa waliozidiwa na kuwapeleka katika hospitali kubwa kwa haraka hasa wanawake ili kupunguza vifo vya kina mama na watoto na kuwataka waitunze pikipiki hiyo

Naye diwani wa kata ya Mfumbi Mh. Athilio Ng'ondya  ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete akiongea kwa niaba  ya wananchi ameishukuru serikali kupitia idara ya afya Makete kwa kuamua kuwapa pikipiki na kuahidi kuwa wataitunza na kuitumia vizuri  kwa kila mtu bila kujali kipato cha mtu wala cheo 

Na: Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo