WAATHIRIKA WA MABOMU YA MBAGALA KUANZA KULIPWA NA SERIKALI

Na Christina Mwagala.
 
SERIKALI imekusudia kuwalipa waathirika 1788 wa mabomu ya mbagala wilayani Temeke jijini Dar es Salaam shilingi bilioni 2.2 kama fidia.
 
Hatua ya kulipwa waathirika hapo imekuja hivi karibuni  kutokana na malalamiko yao kuwasilishwa kwa Serikali baada ya kuona kuwa walikuwa wamesahaulika.
 
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana Mkuu wa Mkoa Said Meck Sadiki alisema waathirika hao watalipwa Jumatatu.
 
Aidha  Sadiki alisema kuwa  wathirika 2132 ndio walikuwa wakidai fidia  lakini kutokana na tathimini iliyofanywa imeonekana kuwa wathirika 1788 ndio wanao stahili kulipwa huku wengine  344 ha watalipwa kwakile kilichodaiwa kuwa walishalipwa tangu hapo awali.
 
Sadiki alieleza kuwa majina ya watako lipwa fidia  ya tabandikwa kwenye mabango ya serikli za kata huku akiwataka wahusika watakaoona majina yao kwenda navitambulisho pamoja na kumbukumbu alizonazo zitakazowezesha dawati la malipo kufanyakazi kwa urahisi.
 
Aidha Sadiki amemtaka mkurugenzi wa halimashauri ya manispaa yatemeke kutoa matangazo kwanjia ya vipaza sauti katika maeneu husika ilikuwafahamisha wanachi juu yazoezi hilo.
 
Tukio hilo lilitokea aprili 2009 katika kambi ya jeshi la ulinzi la wananchi(JWTZ)ambapo mabo hayo yalilipuka mfululizo nakusababisha vifo vya watu zaidi ya 20 na kujeruhi 200 huku mamia ya watu wakikosa makazi hali iliyosababisha watoto wengi kupotea.
 
Hata hivyo mbali watu kupoteza maisha katika tukio hilo pia mabomu hayo yalisababisha uharibifu wakazi yawatu katika eneo hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo