Mkurugenzi amuagiza mratibu wa Tasaf kuwadanganya wanahabari.

Na Kenneth Ngelesi, Mbeya

LICHA ya Rais Jakaya Kikwete kuwaagiza wakuu wa idara kutoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya miradi ya Serikari hali hiyo imekuwa kinyume kwa halmashauri ya Mbeya vijijini  baada ya Kaimu Mkurugenzi   Juliana Lundama kumtaka  mratibu wa TASAF, Hadson Mwasanyamba  atoe taarifa za uongo kwa  vyombo vya habari.

Hali hiyo  imetokea jana katika ofisi za Halmashauri ya Mbeya Vijijni baada ya waandishi kufika katika ofisi za Mkurugenzi kwa lengo la kutaka kupata taarifa za utekelezaji wa miradi mabalimblia ya maendeleo inayosimamiwa na mfuko wa maendeleo wa TASAF.

Baada ya kufika katika ofisi hizo, Lundama alidai kuwa hana taarifa zozote za utekelezaji  wa miradi kwani yeye ana muda mfupi tangu kukaima nafasi hiyo  iliyoachwa wazi kutokana na Mkurugenzi aliyekuja badala ya Juliana malange kuhamishiwa Halmashauri ya Moshi  kurudi halmashauri kwake kwa ajili ya kukabidhi.

Kaimu huiyo aliwataka waandishi wa habari hao waenda kwa wakuu wa idara ili kupatiwa taarifa sahihi jambo ambalo lilikuwa ni danganya toto.

Baadhi ya waandishi  walifika katika ofisi za TASAF na kukutana na mkuu huyo wa idara ambaye alisema   ili aweze kutoa taarifa za utekezaji wa miradi hiyo anaitaji kujiridhisha kwa kupata  ruhusa kutoka kwa mkuu wake wa kazi.

Katika hali ya kushangazwa, Mkuu huyo akiwa anawasiliana na mratibu wa Tasaf kwa njia ya simu ya kiganjani, sauti ya simu hiyo ikiwa juu (Loud speker) sauti ya Kiongozi huyo ilisikika ikimtaka kiongozi huyo kuwadanganya waajndishi hao.

 “ Waandishi hao wamekuja ofisini  kwangu  kutaka taarifa mbalimbali zinazo husu miradi ya maendeleo lakini nimewaeleza kwamba wawaone wakuu wa idara husika kwani ndio wanahizo taarifa kwani mimi sina taarifa sahihi kwa hiyo angalia namna ya kuwa danganya” ilisikika sauti ya Kaimu Mkurugenzi huyo. 

Hatua hiyo imekuwa kinyume na maagizo ya Rais  Jakaya  Kikwete na Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dr Nomad Sigalla aliye wataka watumishi wa serikari kutoa taarifa kwa wana habari hasa juu ya utekezaji wa miradi ya maendeleo inayo simamamiwa na serikari.

Mkuu wa mpya wa wilya ya Mbeya Dr Nomadi Sigala wakati akijitambulisha kwa wakuu wa idara hivi karibuni aliwataka wakuu wa idara kufanya kazi na waandishi wa habari kwani ndiyo njia pekee ya kuwafamisha wanachi kujua nini serikari yao inafanya.

Mwisho


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo