Maiti kumi kati ya kumi na tatu zatambuliwa-Mbeya

Na Kenneth Ngelesi, Mbeya

MIILI  ya watu kumi kati ya kumi na watatu, waliofariki katika ajali mbaya iliyotokea kwenye kona iliyopo mlima Mzalendo, kijiji cha Ntangano-Ijombe, imetambuliwa.

Ajali hiyo iliyotolkea juzi majira ya  saa 7:50 mchana, ilihusisha  gari T.886 BDZ aina ya Toyota Coaster lililokuwa limebeba abiria likielekea wilayani Kyela na gari T.658 ASJ aina ya FAW likiwa na tela T.150 ASN, lililokuwa linatokea mpaka wa Kasumulu, wilayani Kyela.

Muuguzi mkuu wa hospitali ya Rufaha  Mbeya, Thomas Isdory, alisema hadi sasa majeruhi saba wa ajali hiyo bado wanaendelea kupatiwa matibabu na hali zao zinazidi kuimarika tofauti na walivyokuwa wamefikishwa siku ya tukio.

Isdory aliwataja marehemu waliotambuliwa kuwa ni Lucia Livingstone (51), mkazi wa Katumba, Elenesta Kikanga (62), ambaye ni mwalimu mstaafu na mkazi wa Ifunda mkoani Iringa.

Wengine ni Emmanuel Mwanjanja, mkazi wa Ilomba, Pius Beye, mkazi wa Uyole, Mwase Pius, mkazi wa Ilomba jijini Mbeya na dereva aliyekuwa anaendesha basi aina ya Coaster, Mwasa Daimond, mkazi wa Iganzo jiji Mbeya.

Katika hatua nhingine muuguzi huyo aliwataja marehemu wengine kuwa Lenah Ngomano (49), mkazi wa Rungwe, Bahati Jafari (33), mkazi wa wilaya ya Kyela, Mwaniwe Fukasi (35), mkazi wa Uyole mjini Mbeya na Yerusalem Mwakyusa (35), mkazi wa Mbeya mjini.

Muuguzi huoy mkuu  aliwataja majeruhi wanaoendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo kuwa Ford Mwakabungu (35), mkazi wa Kyela, Zainabu Bahati (33), mkazi wa Igawilo na Catherine Komba (23), mkazi wa Hawelo.

Majeruhi wengine ni Neema Mwakalukwa, mkazi wa Mlowo wilayani Mbozi, Paulina Francis (42), mkazi wa Uyole, Esther Mgaya (21), mkazi wa Ujuni na Veronica Charles (57) mkazi wa mkoani Iringa.

“Kwa kweli hali za majerui zinaendelea vizuri ukilinganisha na huziu wakati wana letwa wengi wao hali zao zilikuwa mbaya na bado wanaendelea kupatiwa matibabu” alisema Isdory.

eddymoblaze.blogspot.com  ilifika katika  hospitalini hiyo na  kushushuhudia umati mkubwa wa wananchi waliokuwa wamefika kuchukua miili ya ndugu zao na wengine kuja kuwatambua marehemu, hali iliyopelekea eneo hilo kugubikwa na majonzi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo