Mbunge
wa Jimbo la Ubungo kwa Tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), Mh. John Mnyika (wa pili kushoto) akisubiri
kusomewa hukumu katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam
leo huku akiwa amekaa sambamba na mpinzani wake kwa tiketi
ya CCM Bi. Hawa Ng’umbi (wa tatu kushoto).
Mashabiki
wa Chama cha CHADEMA wakiwa wamefurika ndani ya Mahakama kuu jijini Dar
es Salaam kusikiliza hukumu ya kesi ya Mh. John Mnyika.
Wengine
walikosa nafasi na kuamua kusimama nje ya Lango kuu la Mahakama kuu
Kanda ya Dar es Salaam.
Wafuasi
wa Chama cha CHADEMA wakimpongeza Mh. John Mnyika mara baada ya kuibuka
mshindi dhidi ya kesi iliyokuwa ikimkabili.
Mh.
John Mnyika akiwa amebebwa juu juu na wafuasi wa Chama hicho pamoja na
mashabiki wake nje ya Mahakama Kuu jijini Dar mara baada ya kushinda
kesi yake iliyokuwa ikimkabili kuhusiana na Ushindi wake kwenye uchaguzi
mkuu wa mwaka 2010.
“Pole
sana Mama ndio Siasa hiyo” Mmoja wa Wafuasi wa Chama cha Mapinduzi
akimpa pole Bi. Hawa Ng’umbi (katikati) mara baada ya kutoka Mahakamani.
Wafuasi
wa Chama cha Mapinduzi wakiwa na sura za huzuni baada ya kutoka
Mahakamani.
Mwenyekiti
wa Chama cha CHADEMA Mh. Freeman Mbowe akifunguka na kuelezea furaha
yake wakati wa mahojiano na Mwandishi wa ITV Godfrey Monyo nje ya
Mahakama kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.
Maandamano
ya wafuasi wa CHADEMA wakishangilia ushindi wa Mbunge John Mnyika
wakielekea katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho.
Mh.
John Mnyika ameshinda kesi ya kupinga ushindi wake katika Jimbo la
Ubungo katika hukumu iliyotolewa leo na mahakama kuu ya Tanzania na
kukifanya chama cha CHADEMA kuendelea kushikilia jimbo hilo.
Picha & Story kwa hisani ya MO Blog