NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE - MONDULI
Imeelezwa kuwa kwa sasa idadi ya wanawake kutoka jamii ya wafugaji ambao
wanajitokeza kuwania nafasi za uongozi mbalimbali katika jamii
imefikia asilimia 50 tofauti na hapo awali ambapo wanawake walikuwa na
mwitikio mdogo.
Hayo yameelezwa na Katibu wa umoja wa wanawake kupitia chama cha
mapinduzi(UWT) katika kata ya Engutoto, Bi Bihulda Kisaka wakati
aliopokuwa akiongea na Waandishi wa habari wilayani Monduli
Bi Kisaka alisema kuwa kilichofanya wanawake wengi wajitokeze hasa
katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho ni pamoja na uhamasishaji
ambao unafanywa na UWT wilaya ya monduli
Alifafanua kuwa kuongezeka kwa idadi ya wanawake hasa katika kata ya
Engutoto ni Motisha kubwa sana hasa kwa kata nyingine na jambo hilo
linatakiwa kuigwa na watu wengine
“Tuna idadi kubwa sana ya wanawake wa jamii ya wafugaji ambao
wanajitokeza katika kuomba nafasi mbalimbali tofauti na hapo awali
ambapo wengi walikuwa wanaogopa sana lakini sasa wengi wanajitokeza
sana”alisema Bi Kisaka
Pia aliongeza kuwa pamoja na kuwa wanawake wengi walikuwa wanajitokeza
hasa katika kata hiyo ya Engutoto bado wanawake wanakabiliwa na
changamoto lukuki hali ambayo inachangia hata baadhi yao kushindwa
kutumia demokrasia yao vema
Mbali na hayo alitaja changamoto nyingine ni pamoja na uhaba wa fedha
hali ambayo nayo inachangia kwa kiwango kikubwa sana washindwe kufikia
malengo yao mbalimbali hasa kwenye ulipaji wa ada
Awali aliwataka wanawake kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi zao vema
kwa kujitokeza kwa wingi katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi
kwa kuwa wanahaki zao za msingi.
wanajitokeza kuwania nafasi za uongozi mbalimbali katika jamii
imefikia asilimia 50 tofauti na hapo awali ambapo wanawake walikuwa na
mwitikio mdogo.
Hayo yameelezwa na Katibu wa umoja wa wanawake kupitia chama cha
mapinduzi(UWT) katika kata ya Engutoto, Bi Bihulda Kisaka wakati
aliopokuwa akiongea na Waandishi wa habari wilayani Monduli
Bi Kisaka alisema kuwa kilichofanya wanawake wengi wajitokeze hasa
katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho ni pamoja na uhamasishaji
ambao unafanywa na UWT wilaya ya monduli
Alifafanua kuwa kuongezeka kwa idadi ya wanawake hasa katika kata ya
Engutoto ni Motisha kubwa sana hasa kwa kata nyingine na jambo hilo
linatakiwa kuigwa na watu wengine
“Tuna idadi kubwa sana ya wanawake wa jamii ya wafugaji ambao
wanajitokeza katika kuomba nafasi mbalimbali tofauti na hapo awali
ambapo wengi walikuwa wanaogopa sana lakini sasa wengi wanajitokeza
sana”alisema Bi Kisaka
Pia aliongeza kuwa pamoja na kuwa wanawake wengi walikuwa wanajitokeza
hasa katika kata hiyo ya Engutoto bado wanawake wanakabiliwa na
changamoto lukuki hali ambayo inachangia hata baadhi yao kushindwa
kutumia demokrasia yao vema
Mbali na hayo alitaja changamoto nyingine ni pamoja na uhaba wa fedha
hali ambayo nayo inachangia kwa kiwango kikubwa sana washindwe kufikia
malengo yao mbalimbali hasa kwenye ulipaji wa ada
Awali aliwataka wanawake kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi zao vema
kwa kujitokeza kwa wingi katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi
kwa kuwa wanahaki zao za msingi.
Na FULLSHANGWE