ELIMU JUU YA UNYANYASAJI WA KIJINSIA KWA WANAFUNZI BADO INAHITAJIKA ZAIDI KWA WANANCHI WA MAKETE

Imeelezwa kuwa ufinyu wa elimu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia katika jamii, ni moja ya visababishi vinavyochangia kwa kasi ukuaji wa vitendo vya unyanyasaji kwa wanafunzi

Hayo yamebainika wakati wanafunzi wa shule ya sekondari Kitulo iliyopo wilayani Makete walipokuwa wakizungumza na mwandishi wetu kuhusiana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinavyofanywa dhidi yao

Wamevitaja vitendo hivyo kuwa ni pamoja na waalimu kufanya ngono na wanafunzi wa kike, wanafunzi wenyewe kufanya ngono wao kwa wao pamoja na wanajamii wengine kuwataka kingono na wengi wao hufanikiwa 

Wamesema ukosefu wa mabweni katika shule yao hupelekea kuongezeka kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwani wanafunzi wengi wanatoka mbali na ilipo shule hiyo hivyo hulazimika kutembea umbali mrefu kwenda na kurudi shule jambo ambalo hupelekea kukumbana na vishawishi vinavyowatka kufanya ngono

"Mfano mimi natoka kule Ikiligano hadai hapa ni zaidi ya saa moja nikitembea sasa hawa madereva bodaboda wanakupa lifti hasa sisi wanafunzi wa kike, na wakati mnaenda anakutongoza sasa mimi siwezi kukataa wakati amenipa lifti yaani inatutesa sana" alisema mwanafunzi mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe

Wameongeza kuwa jamii ikizidi kuelimishwa itapelekea vitendo hivyo kupungua ama kufutika kabisa na kulishukuru shirika la Support Makete To Self Support (SUMASESU) kwa kuzidi kutoa elimu ya kupambana na vitendo hivyo kwa wanajamii na wanafunzi wenyewe programu ijulikanayo kama Shule salama ambayo inazidi kuwasaidia siku hadi siku


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo