Chama cha Sauti ya Umma (SAU) kimempongeza Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika (Pichani) kwa ushindi aliyoupata katika kesi ya ubunge na kumtaka achukulie kama changamoto za kisiasa na wala asijenge chuki dhidi ya yeyote.

Katika taarifa ya Chama hicho iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Mwenyekiti wake Dakta Paul Kyara, imesema SAU wameguswa sana na suala lililotokea katika jimbo hilo kwa sababu ofisi yao ya chama Makao Makuu iko jimbo la Ubungo kwa hiyo Mh. Mnyika ni Mbunge wao na wana imani naye.

Dakta Paul Kyara amesema kwa niaba yake binafsi, viongozi wenzake, wanachama pamoja na wafuasi wa SAU wanachukua nafasi hiyo kumpongeza Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, viongozi wenzake, wanachama wa CHADEMA pamoja na wafuasi wote wa CHADEMA nchi nzima na hasa wakazi wa Jimbo la Ubungo ambao ndio walezi wa Mh.John Mnyika .

 Na.MO BLOG TEAM