Tepe za HIV shuleni Tanzania zakera

 
 

Mwalimu mkuu wa shule moja ameambia BBC kuwa kitendo hicho kilifanyika kufuatia ombi la wazazi kuhakikisha kuwa wanafunzi wagonjwa hawapewi majukumu ambayo huenda yakaathiri afya yao.

Lakini ubaguzi kama huu unakiuka sheria ambao adhabu yake ni kifungo cha miaka mitatu gerezani kulingana na shirika moja la kutetea haki za waathirika wa HIV.

Waziri wa afya amesema hawezi kutoa tamko lolote kuhusu madai hayo hadi uchunguzi utakapofanywa.
Kulingana na shirika la UNAids, takriban asilimia tano ya watu milioni 1.4 nchini Tanzania, wanaishi na virusi vya HIV.

NA BBC
Wanaharakati nchini Tanzania wameelezea kughadhabishwa na hatua ya baadhi ya shule nchini humo kuwataka wanafunzi wanoishi na virusi vya HIV kuvaa riboni nyekundu kwenye sare zao za shule wakiwa shuleni.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo