WIVU WA KIMAPENZI UNAPOZIDI................



Katika mapenzi wivu unahusika kwa asilimia kubwa lakini ukizidi unaweza kuwa matatizo,, kuna tukio limetokea huko mkoani Mara wilayani Bunda  Mfanyabiashara mmoja anadaiwa kumgonga kwa gari mkewe na kumjeruhi kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na wivu wa mapenzi.

 Kamanda wa Polisi mkoani Mara Robert Boaz amesema mwanamke huyo anayeitwa Nasra Mohamed mkazi wa mjini Bunda   alipatwa na mkasa huo ambapo siku ya tukio mwanamume huyo aliyekuwa anaendesha gari yake aina ya Nissan T 400 BBC, alimkuta mke wake akiwa anatembea katika barabara kuu ya Mwanza , Musoma mjini Bunda, Imeelezwa kuwa alipomuona mkewe alisimamisha gari lake na kisha akamuita lakini alipomsogelea aliendesha gari kwa kasi na kumgonga na kuanza kuuburuza mwili wake umbali wa zaidi ya mita 150.

 Baadhi ya mashuhuda walidai kuwa licha ya mwanamume huyo kumgonga mkewe hakusimama na kwamba alilitelekeza gari lake katika kijiji jirani baada ya kupasuka gurudumu moja la mbele.Aidha imedaiwa kuwa mwanaume huyo amekuwa akimtuhumu mke wake kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine mjini hapo. Polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanamsaka mtuhumiwa huyo ili sheria ichukue mkondo wake.


NA ADELA BLOG



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo