TUHUMA ZA KUMUACHIA MTUHUMIWA, POLISI MAKETE WANENA

MAKETE                                    23/02/2012

Jeshi la polisi wilayani Makete limetolea ufafanuzi tuhuma za kumuachia mtuhumiwa wa kesi ya kuwaweka kinyumba wanafunzi wawili wa shule ya sekondari Mwakavuta

Akizungumza na Kitulo fm Afisa upelelezi wa wilaya ASP Gozbert Komba amesema tuhuma hizo siyo sahihi kwa sababu mtuhumiwa aliachiwa kwa dhamana na upelelezi unaendelea 

Malalamiko hayo yaliyolewa na mwananchi ambaye hakupenda kujitambulisha jina lake katika kipindi cha morning power kinachorushwa na kitulo Fm akidai  sababu za wanafunzi kujihusisha  na masuala ya uhusiano ya kimapenzi linatokana na mamlaka za kisheria kutokuwachukulia hatua watuhumiwa wa matukio hayo

Wakati huohuo polisi wametolea ufafanuzi kuwa suala la mvutano kati ya wananchi wa kijiji cha Isapulano na na mkazi wa kijiji hicho Bw.Silivyo Mahenge nakusema kuwa wamekwisha lishughulikia suala hilo na kwa sasa lipo mahakamani


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo