MAKETE

MAKETE                             23.02.2012

Imeelezwa kuwa mvua kubwa zinazoambatana na radi zinazoendelea kunyesha hivi sasa wilayani Makete ni miongoni mwa sababu zilizopelekea kukosekana kwa umeme siku mbili mfululizo Februari 19 na 20 wilayani hapa

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Meneja wa TANESCO wilayani Makete Bw. Zebedayo Gadau amesema mbali na mvua hizo pia baadhi ya wachungaji wa mifugo wamekuwa wakichezea nyaya za umeme kwa kutupa matawi ya miti hali inayopelekea hitilafu ya umeme na umeme kukatika

Pia Gadau alikanusha taarifa zilizozagaa miongoni mwa wananchi kuwa hitilafu hiyo ya umeme ilisababishwa na uwekaji wa transfoma katika chuo cha VETA Makete


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo