Taharuki: yatanda Watu watatu wakifa kwa kula nyama msibani

 


Watu watatu wakiwemo mume na mke wamefariki dunia baada ya kula nyama msibani inayodhaniwa kuwa na vimelea vya ugonjwa wa kimeta katika Kijiji cha Msaranga, Kata ya Kisale Msaranga, Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.


Kufuatia tukio hilo lilitokea Mei 4, watu 188 waliokuwepo msibani hapo tayari wamepewa dawa kinga, huku wengine 15 wakiumwa matumbo, kuhara na kutapika huku baadhi wakihusiaha na maradhi ya mifugo.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, tayari timu ya matabibu kutoka mkoani wapo katika kata hiyo kufuatilia tukio hilo.

Taarifa za tukio hilo zimeibuliwa na Diwani wa kata hiyo, Mathias Assenga aliyesema tukio hilo limezua taharuki katika eneo la hilo kutokana na baadhi ya watu kuendelea kuhara na kwamba wengine walioshiriki katika mazishi hayo wanaendelea kuchunguzwa kwa ukaribu.

"Kulikuwa na mazishi mahali hapa kwenye kata yangu, ambayo yalifanyika kwa mzee mmoja aliyekuwa amefiwa na kijana wake, sasa wakati wa mazishi kuna mama alikuwepo anahudumia kule jikoni, ambaye pia alichukua na chakula na kupeleka nyumbani baada ya shughuli ya mazishi kumalizika.

"Chakula hicho baada ya kupeleka nyumbani alikula yeye na mume wake, mwali wake pamoja na mjukuu wake aliyekuwepo nyumbani hapo siku ya Mei 4.

“Siku iliyofuatia ambayo nilikuwa Ijumaa huyu mama alijisikia vibaya na siku ya Jumapili alipoenda hospitali alizidiwa na Jumatatu ya Mei 8 alifariki dunia.

"Lakini wakati huo tayari mume wake naye alikuwa ameshaanza kuharisha na alikuwa hospitalini na hakuweza kumzika mke wake.Alhamisi ya Mei 11 mume wake naye akafariki na mwali (mkwe) wake naye pia akawa amelazwa hospitalini.”

Alisema kufariki kwa watu hao kumeleta taharuki kubwa kwenye kata hiyo baada ya kijana mwingine aliyekuwa akihudumia chakula katika msiba huo kufariki dunia.

"Sasa hii imeleta taharuki kidogo kwa sababu kuna kijana mwingine wa familia nyingine ambaye naye alikuwa anahudumia pale msibani naye akawa amekufa na alizikwa Mei 17 na wale wote ambao walikuwa wanaharisha walielekezwa kwenda hospitali," alisema.

Alisema katika kata hiyo watu 15 ambao walikuwa wanahara walikwenda hospitali na kupewa tiba na kurudi na kwamba kinachofanyika kwa sasa ni kuendelea kufuatilia hali zao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo