Mhubiri Kizimbani kwa kushiriki ngono na binti wa miaka 14

Mhubiri wa Kanisa la Jesus Revelation Center kutoka kata ya Tezo maeneo ya Mbuyuni nchini Kenya anatarajiwa kufikishwa Mahakamani hii leo kwa tuhuma za kushiriki ngono na mtoto mwenye umri wa miaka 14.


Mchungaji huyo ambaye amezua mijadala mitandaoni kwa kitendo hicho, atafikishwa ili kusomewa shitaka lake huku waumini wake nao wakikumbwa na butwaa kutokana na mfululizo wa matukio ya wahubiri kukubwa na kashfa nzito.

Wakati hilo likitokea, tayari Mchungaji Ezekiel Odero ambaye alihusishwa kushiriki mauaji ya halaiki yaliyotokea shambani mwa Mchungaji mwingine Paul Mackezie wa Kaunti ya Kilifi ameachiwa huru kwa dhamana.

Kwa upande wa Mackenzie yeye alitarajia kupanda kizimbani hii leo kusomewa mashitaka yanayomkabili ya mauaji ya watu zaidi ya 120, akituhumiwa kuwahubiria na kuwataka wafunge kula hadi kufa ili wakakutane na MUNGU wao na huku akiwaaminisha mwisho wa Dunia ni mwaka huu 2023.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo