Shabiki wa Yanga afariki dunia akitazama Dabi ya Kariakoo

Shabiki wa Yanga aitwaye Jane, mkazi wa Kata ya Bwilingu Huko Chalinze mkoa wa Pwani, amepoteza maisha wakati akiangalia mchezo wa jana wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga.


Imeelezwa kuwa shabiki huyo alipatwa na presha na kuanguka ghafla.

Katika mchezo huo uliopigwa Aprili 16, 2023 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ulishuhudia Simba wakimaliza uteja wa miaka mitatu kwa kuitandika Yanga mabao 2-0, ambayo yalipachikwa na Inonga Baka na Kibu Denis.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo