Rais awataka wanaume kuacha kupekua simu za wake zao


Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amewataka raia wa nchini humo kuacha kuchunguza simu za wapenzi wao.


Wito wake ukionekana kuwa sehemu ya ombi la kujaribu kupunguza viwango vya talaka nchini.

Takwimu zinaonyesha kuwa nchi hiyo ilirekodi zaidi ya kesi 22,000 za talaka mwaka jana pekee, takwimu ambazo rais alizitaja kuwa za kusikitisha.

Ukosefu wa haki za ndoa, uzinzi, unyanyasaji wa kijinsia, matusi na ukatili ni miongoni mwa sababu zilizotolewa mahakamani katika kesi zinazohusu talaka.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo