Wazazi Waamua Kulisha Watoto wao Bangi na Pombe Sababu ya Njaa

Wakazi wa kijiji cha Makwa katika eneo la Gatundu Kaskazini, Kaunti ya Kiambu, huwa na matumaini kila wanaposikia mingurumo ya magari ya kutoa chakula cha msaada ili kuwawezesha kukabiliana na ukame unaoendelea kuhatarisha maisha yao.


Lakini jambo la kushangaza ni kwamba athari ya ukame zimewafanya wazazi kubuni njia za ajabu za kutoa matumaini kwa watoto wao. Wazazi hao sasa wanapoesha makali ya njaa kwa kuwalazimisha watoto wao kutumia bangi na pombe ambayo ni ya bei nafuu na inayopatikana kwa urahisi katika kijiji hicho ili kuwazuia kuitisha chakula ambacho kwao ni dhahabu.


Kulingana na wazee wa kijiji hicho, wazazi hao hutumia chang’aa, bangi na dawa zingine za kulevya ambazo hupatikana kwa urahisi.


“Tunasikitishwa na ukweli kwamba baadhi ya wazazi sasa wanaamua kuwapa watoto bangi na vileo vya bei nafuu ili kusahau kula. Mara tu wanapotumia dawa mbalimbali zilizopigwa marufuku, watoto wengi huishia kulala,” Kimani alisema. 


Wakaazi hao wanaokabiliwa na njaa waliiomba serikali kuchangia haraka chakula cha msaada katika eneo hilo ili kuokoa maisha. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo