Askari alivyofariki dunia akilinda mtihani wa Taifa

ASKARI wa Jeshi la Akiba (Mgambo), mkazi wa Kijiji cha Manyoni, Kata ya Misozwe wilayani Muheza mkoani Tanga, Yustino Mhina, amekutwa amefariki dunia kwenye kiti wakati akilinda mtihani wa darasa la saba mwaka huu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Henry Mwaibambe, alithibitisha jana kutokea kwa kifo hicho, akibainisha kuwa askari huyo alikutwa na umauti Alhamisi ya wiki hii, siku ya pili ya mtihani huo wakati watahiniwa wa darasa la saba wakifanya mtihani huo wa kuhitimu elimu ya msingi.

Alisema Mhina alikuwa akilinda mtihani huo katika Shule ya Msingi Lumbizi iliyoko Kijiji cha Kwatango, Kata ya Kwemingoji wilayani hapa.

Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kwemingoji, Levina Mushi, alisema askari huyo ambaye tayari mwili wake umeshazikwa, alibainika kupoteza maisha wakati walinzi wenzake walipomkuta asubuhi akiwa kwenye kiti shuleni huko.

Mtendaji huyo alisema mwili wake ulipelekwa Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza kwa ajili ya uchunguzi na majibu yalionyesha alikunywa dawa zaidi ya kipimo

Alisema mlinzi huyo alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kifafa na alikuwa anatumia dawa kutibu ugonjwa huo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo