Mwanamume aliyetuhumia kuhusika katika mauaji ya binti yake Hakimu wa Mahakama ya Githongo, Caroline Kemei amehukumiwa kifungo cha miaka 40 gerezani.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Chuka, Lucy Gitari alimfunga jela Benson Kimathi, ambaye ni askari jela wa zamani wakati wa kikao cha korti Jumatatu, Oktoba 24.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Chuka, Lucy Gitari alimfunga jela Benson Kimathi, ambaye ni askari jela wa zamani wakati wa kikao cha korti Jumatatu, Oktoba 24.
Kimathi alishtakiwa pamoja na Francis Otundo, ambaye anasemekana alipigia simu familia ya Kemei akiitisha KSh.500,000.
Siku chache baada ya kutoweka, mwili wake Maribel uliokuwa ukioza ulipatikana umetupwa katika msitu wa Gitoro katika kaunti ya Meru nchini Kenya. Otundo aliachiliwa kwa masharti kwa mwaka mmoja baada ya kubainika kuwa alikuwa tu na nia ya kumlaghai mama yake mtoto huyo na wala hakuhusika katika mauaji hayo. Gitari alisema kwa muda ambao amekuwa kizuizini ni funzo kwake na kumwachilia.
Alibainisha kuwa msichana huyo alikufa kifo cha uchungu kwa kosa ambalo hakufanya, na kuongeza kuwa lilistahili adhabu hiyo kali. Mahakama iliambiwa kuwa mshukiwa mkuu na mama yake msichana huyo walikuwa wameachana baada ya kuwa pamoja katika uhusiano ulioshindikana.
Kabla ya hakimu na mshukiwa kuvuna uhusiano, bintiye alikuwa amekaribiana sana na mshukiwa na hata wakati mwingine angemchukua katika kituo cha mafuta cha Meru mjini ambapo basi la Shule ya Msingi ya Consolata lilikuwa likimshusha jioni.
Mtindo huo huo ulitokea Septemba 6, 2018, lakini mshukiwa wakati huo hakumpeleka msichana nyumbani na kusababisha familia yake kuwa na wasiwasi baada ya kushindwa kumpata.
Wanafunzi wenzake wanaoishi karibu walisema msichana huyo alichaguliwa na mtu aliyemtaja kama 'Mjomba', na kwa kuwa haikuwa mara ya kwanza kuwaona pamoja, walifikiri walikuwa na uhusiano wa karibu.
Chanzo: TUKO.co.ke