Wanachadema Jitoeni kuchangia Maendeleo ya Nchi - CHADEMA Makete


WANACHAMA  WA chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wilayani Makete mkoani Njombe wamesisitizwa kuchangia michango mbalimbali ya maendeleo katika maeneo wanayoishi wilayani hapa.

Akizungumza na wanachama wake wa kata ya Ikuwo mwenyekiti chama hicho wilaya ya Makete Ibrahimu Ngogo amesema kama mwenyekiti atafurahishwa kuona wanachadema wanakuwa mstari wa mbele katika shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti Ngongo amesema pasipo kujali kiongozi anayeongoza eneo husika anatoka upande wa chama gani cha siasa, wao wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kuchangia maendeleo.

Amesema chama hicho kimejaliwa watu wachapa kazi hivyo wanatakiwa kuwa mfano katika kupigania maendeleo ili taifa lisonge mbele.

Amesema kiongozi yeyote atakayetangaza michango au shughuli ambazo ziko kinyume na sheria za nchi wanachadema wasisite kuikataa na kuikemea.

Naye mwenyekiti wa madiwani wa Chadema mkoa wa Njombe ambaye pia ni diwani wa kata ya Matamba Mh Ephel Ng’ondya amesema wanachi na wanachama wa chama hicho kata ya Ikuwo wahakikishe wanafanya kazi kwa kushirikiana na diwani wao ili kufanikisha maendeleo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo