Abiria wachoma moto basi walilosafiria

Abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Mombasa kwenda Nairobi nchini Kenya, wamelichoma basi walilokuwa wakisafiria katika eneo la Tajmali huko Embakasi

Chanzo cha abiria hao kufanya hivyo kimeelezwa kuwa ni hasira walizokuwa nazo baada ya dereva kulazimisha kutumia njia ambayo imeathirika na mafuriko, na kuhofia kukaa njiani kwa muda mrefu kutokana na foleni.
Abiria hao walikuwa wakimtaka dereva kutumia njia ya kupitia Outering kwenda Nairobi, badala ya barabara ya Mombasa ambayo dereva alikuwa akisisitiza kuitumia.
Baada ya mvutano wa hapa na pale ndipo abiria hao waliposhikwa na hasira na kuamua kulichoma moto basi hilo na kisha wote kukimbia, na dereva naye kuamua kukimbia eneo la tukio.
Source
Ghetto Radio Kenya
Basi lililochomwa moto na abiria


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo