Taarifa Muhimu Kutoka NACTE Hii leo

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limesema mitihani ya kuhitimu kidato cha sita itaanza Mei 7 hadi 24, 2018.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Necta Januari 26, 2018 inaonyesha somo la kwanza litakuwa ni masomo ya jumla ‘General Studies’ na somo la mwisho litakalofanyika Mei 24 litakuwa ni Baiolojia 3C (kwa vitendo).

Msemaji wa Necta, John Nchimbi amesema “lengo la kutoa ratiba ni kuwafanya wanafunzi na walimu wao kujiandaa kwa ajili ya mitihani yao.”

“Ratiba inawasaidia wao kuweza kufanya maandalizi lakini kuwaweka sawa kisaikolojia  na kujua mitihani ipo, itakuwa lini hadi lini na muda gani,” ameongeza


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo