Madiwani wengine wa CHADEMA Arusha wahamia CCM

Madiwani watatu wa Chadema, katika halmashauri ya Longido mkoa wa Arusha , wametangaza kujiuzulu na kujiunga na Chama cha Mapinduzi ( CCM).

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Longido, Jumaa Mhina alithibitisha leo Januari 10 kujiuzulu kwa madiwani hao, Jacob Silas Mollel Kata ya Elang'atadapash, Elias Mepukori Mbao Kata ya Kamwaga na Diyoo Lomayani Laizer Kata ya Olmolog.

Mhina amesema sababu za kujiuzulu madiwani hao wamezitoa kuwa ni kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli katika vita dhidi ya ufisadi, kuinua uchumi na pia kurejesha nidhamu kazini.

"Tayari tumepokea barua zao na tumezipeleka TAMISEMI kwa ajili ya utaratibu wa kisheria ili kuwezesha kufanyika uchaguzi mdogo baada ya Tume kupata taarifa" Amesema

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Longido, Onesmo ole Nangole pia amethibitisha kuondoka kwa madiwani hao na kueleza chama hicho, kinafuatilia tukio hilo.


Madiwani hao kujiunga na CCM wanafanya mkoa wa Arusha pekee kuwa na jumla ya madiwani 13 wa Chadema ambao wamejiuzulu na kujiunga na CCM tangu kumalizika uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Na Mussa Juma, Mwananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo