Walimu watarajiwa Chuo cha Ualimu Tandala Wapewa Onyo

Wito umetolewa kwa Wahitimu wa mafunzo ya ualimu mwaka wapili na watatu katika chuo cha ualimu Tandala  kuwa mfano mwema katika jamii kwa kufanya matendo mema pindi wanapohitimu chuoni hapo
Wito huo umetolewa na mgeni rasmi Afisa elimu sekondari wilaya ya Makete Jackobo Meena katika mahafali ya 41 kwa walimu wa awali  na msingi  ambapo amesema wahitimu hao wanatakiwa kufanya mambo mazuri katika jamii na kutojiingiza kuwa watenda maovu huku akiwakumbusha kuwa mwalimu ni kioo cha jamii
Awali wakisoma Risala kwa mgeni rasmi wahitimu hao wamezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili kama uhaba wa vyumba vya madarasa, maktaba viwanja vya michezo, kukosa zahanati, usafiri  pamoja na chumba cha ITC
Akimkaribisha mgeni rasmi, makamu mkuu wa chuo hicho amewapongeza wahitimu na kuwatakia maisha mema huku akiwasisitizia nidhamu na maadili kwa pamoja na uwajibikaji
mahafali hayo ni ya  41  ambapo wahitimu  186 wamehitimu katika ualimu msingi yaani ordnary diploma in primary education na ualimu awali yaani odinary in Early childhood care and education

Na Riziki Manfred


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo