Tunajua walikokimbilia - IGP Sirro

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Siro amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi nchini linataarifa za kutosha kuhusu sehemu ambayo wamekimbilia wahalifu waliokuwa wakifanya mauaji mkoani Pwani katika maeneo ya Kibiti

IGP Sirro amesema hayo leo alipokuwa mkoani Mtwara na kuwataka wahalifu hao waliokimbilia mkoani Mtwara kuacha mara moja vitendo vya uhalifu walivyokuwa wakifanya Kibiti kabla ya jeshi la polisi kuwatia nguvuni.
Mkoani Pwani zaidi ya watu 30 walifariki dunia wakiwepo viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi, askari polisi na raia wengine kwa kuuwawa na watu wasiojulikana ambao walikuwa wakifanya uhalifu huo na baadaye kuzibitiwa na jeshi la polisi huku wahalifu wengine wakisemekana kukimbia katika maeneo hayo na kukimbilia mkoani Mtwara 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo