Rais Magufuli amepotoshwa

Umoja wa mawakala wa pembejeo za kilimo nchini wamemuomba Rais John Pombe Magufuli kukutana nao ili kuweza kulipatia suluhu suala linalowakabili la madai ya fedha wanazoidai serikali kwa ajili ya usambazaji wa pembejeo katika msimu wa mwaka 2015/2016

Maombi ya kukutana na Rais Magufuli yametolewa leo na Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakala wa pembejeo za kilimo nchini ndugu, Gerald Mlenge wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu malalamiko ya madai yao kwa serikali ili Rais Magufuli aweze kuelezwa ukweli na aweze kutoa ufumbuzi wa jambo lao hilo. 
"Rais Magufuli tafadhali kama unatusikia tunakwambia juu ya zoezi hili na jinsi linavyoendeshwa ukweli tunao sisi mawakala, tunaoitwa wezi badala ya kutuambia kuwa wadanganyifu sasa wewe utuite tukwambie na mengine Mhe. Rais tunakuomba, tunaomba viongozi wote wa Wizara ya Kilimo hasa wale wasimamizi wa kitengo cha pembejeo za ruzuku katika kikao chako nao wawepo ili tuongee yote ya moyoni ili wewe uweze kutoa maamuzi yako kwa haki juu ya malipo yetu sisi tunaoteseka" alisema Gerald Mlenge 
Hata hivyo Makamu Mwenyekiti wa umoja huo Idd Madeni amesisitiza kuwa wao wana mambo mengi ya kusema lakini hawana sehemu ya kusema mambo ambayo wanakutana nayo 
"Tuna mengi ya kusema lakini hatuna sehemu ya kusemea, tunaiomba serikali yetu tunaamini ni sikivu itatusikia, mfumo ulipangwa na serikali mimi ni mtu wa mwisho lakini hakuna hata siku moja kiongozi yoyote ngazi yoyote ambaye amedai, ameshtakiwa, ambaye ameambiwa mbadhilifu au mwizi zaidi ya yule wa chini" alisisitiza Idd Madeni 
Mwezi Julai Rais Magufuli alisema kuwa amegundua kuna ubadhilifu mkubwa wa fedha kwenye pembejeo na kudai hata huko kuna hewa nyingi na kuagiza uchunguzi uweze kufanyika ili kuweza kubaini hewa hizo. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo