Marufuku kuosha magari

Related image
Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam imesema kila kijana atakayekutwa anaosha magari pembezoni mwa barabara za manispaa hiyo atapigwa faini ya shilingi laki mbili papo hapo huku mmiliki wa gari husika nae akitozwa faini kama hiyo.

Aidha Mkurugenzi wa mazingira amesema licha ya kupigwa faini kwa watu hao lakini bado watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
Mkuruegenzi wa mazingira na udhibiti wa taka katika manispaa ya Ilala Bw. Abdon Mapunda amesema kumezuka tabia kwa baadhi ya vijana kugeuza maeneo mbali mbali ya manispaa hiyo kuwa maeneo ya kuosha magari huku maji wanayotumia yakitiririka barabarani na kusababisha kutuama jambo ambalo ni uchafuzi wa mazingira.
Amesema tangu kuanza kwa zoezi hilo mwezi Juni mwaka huu wameshafanikiwa kukamata vijana hao pamoja na wamiliki wa magari wasiopungua 50 na kuwapiga faini pamoja na kuwafikisha mahakamani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo