Masauni: Lazima tushinde vita ya Kibiti

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Hamad Masauni amesema kuwa Suala la kumaliza uhalifu kibiti na Mkuranga ni jambo ambalo halina mjadala kwani ni lazima lidhibitiwe.

Mhe. Masauni amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mauaji yanayoendelea maeneo ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga.

“Suala la kumaliza uhalifu Kibiti na Mkuranga ni suala ambalo halina mjadala, ni suala la lazima lakini, suala ni lini uharaka wake ndio maana tumejadili changamoto zinazokabili ili tuweze kukaa kwa pamoja tuweze kuzifanyia kazi. Tuweze kuharakisha zoezi hili ambalo kwa hakika kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa sisi tunaosimamia haki na uhai wa raia wasio kuwa na hatia hii vita lazima tushinde inshaallah,” alisema Masauni.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo