CHADEMA wameeleza kuhusu Lowassa kuitwa kwenye mahojiano Polisi

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Waziri Mkuu Mstaafu,  Edward Lowassa amepata wito kutoka kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kumtaka kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kesho Jumanne, saa 4 asubuhi kwa ajili ya mahojiano. 
Taarifa iliyotolewa na CHADEMA imesema kuwa  hajapewa maelezo wala ufafanuzi wowote kuwa mahojiano hayo yatahusu nini hasa.
CHADEMA wameeleza kuwa taarifa za awali zinaonesha kuwa mahojiano hayo yanahusishwa na kauli za Lowassa alizotoa katika nyakati tofauti hivi karibuni wakati akishiriki futari katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Kwenye vyombo vya habari leo Lowassa ameripotiwa akimtaka Rais Magufuli kuwaachia huru mashehe wa uamsho ambao inadaiwa wanashikiliwa kwa miaka minne sasa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo