Mwanafunzi wa shule ya msingi Matwiga Wilayani Chunya, Mkoani Mbeya aliyetambulika kwa jina la Daudi Kaila amefariki dunia baada ya kufungiwa katika chumba cha stoo ya shule na mwalimu Mkuu wao.
Inasemekana Mwalimu Mkuu huyo aliwafungia wanafunzi wawili kwa zaidi ya masaa mawili kwenye chumba hicho cha stoo akiwepo Daudi Kaila na mwenzake Felix Samweli ambaye yeye amenusurika kifo. Sababu kubwa mwalimu kuwafungia wanafunzi hao ilikuwa kuwaadhibu kutokana na wanafunzi hao kutohudhuria shule kwa siku tano.
Kufuatia tukio hilo kutokea walimu wa shule hiyo wamekimbia kusikojulikana kuokoa maisha yao kutoka kwa wananchi wenye hasira kali
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi