AUDIO: Aliyoyasema Waziri Mwakyembe baada ya Kukutana na Nape

Waziri mpya wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amewataka wanamichezo kumpa ushirikiano katika kuendeleza gurudumu la maendeleo.
Dk Mwakyembe ambaye amechukua nafasi ya Nape Nnauye amesema anaweza kufanya vizuri kama watashirikiana pamoja na wadau wa michezo.

“Tukishirikiana kila jambo litaenda vizuri, serikali inataka mabadiliko, inataka mafanikio na hii ni kwa faida ya wanamichezo. Tushirikiane,” alisema.

Jana, Dk Mwakyembe alikaa kikao cha kwanza cha Kamati ya Serengeti Boys na baadaye akaenda Uwanja wa Taifa kuiunga mkono Taifa Stars iliyokuwa inacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Botswana na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, yote yakifungwa na nahodha Mbwana Samatta.

Sikiliza Sauti hii aliyoyasema


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo