Baba amvunja Mwanae Mkono....Ni baada ya Kuchelewa kutoka Shuleni

Uongozi wa serikali ya kijiji cha Korini kusini wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro unamsaka mkazi wa kijiji hicho Deo Manga kwa tuhuma ya ukatili dhidi ya mwanae Dorini Manga kwa kumvunja mkono wa Kushoto

Mtoto Dorini Ni mwanafunzi wa darasa la Kwanza katika shule ya msingi Kiwalaa na alichapwa fimbo na baba yake mzazi hadi mkono kuvunjika na kisha baba yake kutokomea

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi anakosoma mtoto huyo Evance Tarimo amekiri kutokea kwa tukio hilo

Mtoto Dorini ameelezea sababu za kufanyiwa ukatili huo na baba yake mzazi kuwa ni kuchelewa kutoka shuleni


Mwenyekiti wa kijiji hicho Emanuel Mrema ameahidi mtuhumiwa huyo kukamatwa ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazomkabili


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo