AUDIO: Miti zaidi ya 600 ya Mapambo Yapandwa Makete Mjini Leo

Mkuu wa wilaya ya Makete mkoani Njombe Mh Veronica Kessy leo amewaongoza wananchi wa mji mdogo wa Iwawa katika uzinduzi wa zoezi la upandaji miti katika mji huo ambapo shughuli kubwa ilikuwa kupanda miti ya maua na mapambo

Lengo la upandaji miti hiyo ambayo ni ya kivuli na yenye kupendezesha mji, ni kuhakikisha mji mdogo wa Iwawa unakuwa na muonekano mzuri kwa kuwa uko wazi kutokana na kutopandwa miti, hivyo miti hiyo iliyopandwa itasaidia kupunguza athari mbalimbali zitokanazo na upepo mkali mathalani kimbunga

Akizungumzia zoezi hilo Afisa Mazingira Bw. Raphael Kalongola amesema Zaidi ya miti 600 imepandwa ambayo ni ya aina tofauti tofauti yenye kupendezesha mji, ambapo mbali na mkuu wa wilaya ambaye alikuwa mgeni rasmi kushiriki, pia viongozi wengine ngazi ya wilaya pamoja na wananchi wameshiriki zoezi hilo

Amesema katika mji mdogo wa Iwawa kuna maeneo mengine ambayo bado miti haijapandwa na kwa kuwa zoezi hilo ni endelevu mpaka Machi Mwaka huu, hadi kufikia kipindi hicho miti itakuwa imepandwa kama ilivyokusudiwa

Bw. Kalongola amewaomba wananchi kuitunza miti hiyo kwani mbali na kusaidia kupendezesha mandhari ya mji, lakini pia miche ya miti hiyo inauzwa ghali na kutolea mfano baadhi ya miti mche mmoja kuuzwa shilingi 20,000/= na wao kama halmashauri wamekusudia kuikabidhi miti hiyo kwa watu ambao wataandikishwa majina kama njia rahisi ya kuitunza

Sikiliza sauti hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo