Mkuu wa Wilaya Aagiza aliyejificha Msituni asakwe Mpaka apatikane

MKUU wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa ,Said Mtanda amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo , Julius Kaondo kuhakikisha inamsaka, kumkamata na kumfikisha mahakamani ‘mvamizi’ anayendelea kuishi kwa kificho ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Mfili.
Mtanda, alitoa  agizo hilo  mbele ya   Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya  Makazi, Angelina Mabula alipokutana na watumishi wa halmashauri hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Ninazo taarifa, licha ya operesheni tuliyoifanya siku tatu kuwaondoa wavamizi waliokuwa  wakiishi  na kufanya  shughuli za kibinadamu  ndani ya msitu huu, bado yupo mtu amejificha  na anaendelea kuishi ndani ya msitu huo ….
Sasa namwagiza mkurugenzi mtu huyo asakwe, akikamatwa hakikisha
anafikishwa mahakamani  ili sheria iweze kuchukua mkondo wake,”alisisitiza .
Alisema  ni marufuku kwa mtu yeyote  kuishi na kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya msitu huo na  atakayekaidi  atajutaa yake .Alisisitiza kuwa  msitu huo ni eneo oevu   umehifadhiwa kihalali kupitia sheria ndogo ya mwaka 1998 .
Alisema  mwezi uliopita aliongoza operesheni maalumu  ambapo wavamizi wote waliokuwa  waiishi kinyume cha sheria katika msitu huo, waliondolewa, huku nyumba na mashamba  vikiteketezwa kwa moto .
Naibu Waziri,Angelina  aliwataka wananchi kuhakikisha msitu huo, unalindwa kwa sababu  ni chanzo pekee cha maji kinachotegemewa na wakazi wa mji wa Namanyere.
Na Gurian  Adolf-Nkasi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo