AUDIO: Ufafanuzi Kuhusu Mwalimu Mkuu Kukutwa na Vyeti Feki Makete

Afisa elimu shule za msingi wilaya ya Makete Mwl.Antony Mpiluka ametolea ufafanuzi juu ya taarifa zilizokuwa zikienezwa kuwa aliyekuwa Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Missiwa iliyopo katika kata ya Ipelele wilayani Makete Bi.Gloria Simba ametoroka na kuitelekeza shule hiyo kwa kuhofia kutumbuliwa kutokana na kughushi vyeti vyake vya kazi na kubainisha kuwa mkuu huyo wa shule amehamishwa kwa taratibu kwenda shule ya msingi Ruaha ambayo ni shule mpya.

Mwl.Mpiluka ametoa ufafanuzi huo leo alipokuwa akizungumza na kituo cha redio Green Fm kwa njia ya simu katika mahojiano maalum,ambapo amekanusha taarifa hizo huku pia akimtaja Furaha Fungo kuwa ndiye atakuwa mbadala wa mkuu huyo wa shule.

Pia Mwl.Mpiluka ameelezea kusikitishwa kwake kufuatia shule za msingi za kata ya Ipelele iliyopo katika tarafa ya Magoma wilayani hapa kufanya vibaya katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu kama anavyoeleza.

Mwl.Mpiluka pia akaelezea hali halisi ya matokeo ya darasa la saba mwaka huu huku akidai kuwa kiwango cha ufaulu kimeshuka kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka jana.

Mwl.Mpiluka ametumia fursa hiyo pia kuzitaja shule 10 bora kwa wilaya ya Makete zilizofanya vizuri kwa matokeo ya darasa la saba mwaka huu na shule 20 zilizofanya vibaya katika matokeo hayo.

Na Fadhili Lunati

Sikiliza sauti yake hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo