Halmashauri ya wilaya ya Makete Mkoani Njombe imeendelea na ufumbuzi wa kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wake hasa kuimarisha barabara zilizoko chini yake kabla msimu wa mvua haujaanza
Hivi sasa halmashauri hiyo imeanza ukarabati wa barabara ya kuelekea hospitali ya Consolata Ikonda kwa kuiwekea kifusi kizuri na imara ili barabara hiyo yenye matumizi makubwa kutokana na hospitali hiyo iendelee kupitika misimu yote ya Mwaka
Mwandishi wetu hii leo amepita katika barabara hiyo na kushuhudia malori yakimwaga kifusi hatua inayoashiria ni mwanzo mzuri wa Matengenezo hayo
Hivi karibuni Mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi alitangaza hadharani katika mkutano na wananchi wa kata ya Tandala kuwa wakati wa ujenzi wa barabara ya Makete Njombe kwa kiwango cha lami utakapofanyika barabara hiyo ya kuelekea hospitali ya Ikonda nayo itajengwa kwa lami na serikali ya awamu ya 5




