Mkuu wa Wilaya ya Arusha mteule Bw. Gabriel Fabian Dagarro
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe
21 Agosti, 2016 amemteua Bw. Gabriel Fabian Daqarro kuwa Mkuu wa Wilaya
ya Arusha.
Bw.
Gabriel Fabian Daqarro anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Mrisho
Mashaka Gambo ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Uteuzi wa Bw. Gabriel Fabian Daqarro unaanza mara moja.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
21 Agosti, 2016
