Zitto Kabwe aitwa na Hillary Clinton Marekani

Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameondoka nchini kuelekea Philadelphia nchini Marekani kuhudhuria mkutano mkuu wa chama cha Democrats utakaomthibitisha Bi. Hillary Clinton kuwa mgombea urais kupitia chama hicho.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya ACT Wazalendo wakati akiwa kwenye mkutano huo ndugu zitto atapata fursa ya kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa kisiasa duniani.

Shughuli nyingine atakayofanya ni pamoja na kufanya kikao cha maandalizi juu ya ufunguzi wa tawi la wanachama wa ACT Diaspora la nchini Marekani pamoja na kuwa na mazungumzo maalumu na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Shariff Hamad juu ya hali ya kisiasa ya zanzibar na taifa kwa ujumla.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo