skip to main |
skip to sidebar
Afariki baada ya kurukiwa na samaki Ziwa Nyasa
Mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Kanga, kata ya Ipinda katika Wilaya ya
Kyela mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kurukiwa na samaki aina ya
Perege mdomoni wakati akiwa anavua samaki ndani ya Ziwa Nyasa.
Marehemu aliyefahamika kwa jina la Robert Mwaijenga mwenye umri wa miaka
47, alirukiwa na samaki huyo ambaye baadaye alikwama shingoni mwake na
kumsababishia kifo.
Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho Mganga mkuu wa Kituo cha Afya cha
Ipinda Dokta, FRANK MWAKALUNDWA, amekiri kumkuta samaki shingoni mwa
marehemu baada ya kumfanyia upasuaji.
Mwenyekiti wa kijiji hicho SAMWEL MWAKAJUNGWA, amekiri kutokea kwa tukio
hilo huku shuhuda wa tukio hilo EMMANUEL MWAMGUNDA, akieleza kuwa
lilimpata wakati akiwa kwenye shughuli za uvuvi kwenye Ziwa Nyasa.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi