Upungufu wa madawati 40 katika shule ya msingi Tandala Mazoezi iliyopo katika kijiji cha Tandala kata ya Tandala wilayani Makete umepelekea kuitishwa kwa mkutano wa dharura wa kijiji cha Tandala ili kujadiliana jinsi ya kumaliza tatizo hilo la madawati
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Yoanesi Chaula amesema hapo awali shule hiyo haikuwa na upungufu wa madawati lakini baada ya wataalamu wa elimu kuja na kufanya ukaguzi katika shule hiyo na kuelekeza kuwa kila dawati inatakiwa wakae wanafunzi wawili hali hiyo imepelekea upungufu wa madawati 40 katika shule hiyo.
Aidha mwalimu mkuu huyo amewasihi wananchi wote kuwa suala la kuchangia elimu ni la wanajamii wote bila kujali kama anamtoto anayesoma katika shule hiyo ama la kwani kuchangia maendeleo ni suala la jamii kwa ujumla.
Wakitoa maoni yao kuhusu kuchangia mchango huo wananchi wa wameonekana kuwa na hamasa kubwa ya kuchangia mchango huo kwani hawapo tayari kuwaona wanafunzi ambao ni taifa la kesho wakisomea katika mazingira magumu na kukubaliana kuchangia shilingi 2000 kwa kila mwananchi.
Mwenyekiti wa kijiji cha Tandala Andowise Memba ametolea ufafanuzi kuhusu mchango huo na kwamba wamekubaliana baada ya wiki mbili kila mwananchi awe ameshatoa mchango huo.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Yoanesi Chaula amesema hapo awali shule hiyo haikuwa na upungufu wa madawati lakini baada ya wataalamu wa elimu kuja na kufanya ukaguzi katika shule hiyo na kuelekeza kuwa kila dawati inatakiwa wakae wanafunzi wawili hali hiyo imepelekea upungufu wa madawati 40 katika shule hiyo.
Aidha mwalimu mkuu huyo amewasihi wananchi wote kuwa suala la kuchangia elimu ni la wanajamii wote bila kujali kama anamtoto anayesoma katika shule hiyo ama la kwani kuchangia maendeleo ni suala la jamii kwa ujumla.
Wakitoa maoni yao kuhusu kuchangia mchango huo wananchi wa wameonekana kuwa na hamasa kubwa ya kuchangia mchango huo kwani hawapo tayari kuwaona wanafunzi ambao ni taifa la kesho wakisomea katika mazingira magumu na kukubaliana kuchangia shilingi 2000 kwa kila mwananchi.
Mwenyekiti wa kijiji cha Tandala Andowise Memba ametolea ufafanuzi kuhusu mchango huo na kwamba wamekubaliana baada ya wiki mbili kila mwananchi awe ameshatoa mchango huo.

