Watu watano wamefariki dunia papo hapo na wengine 35 kujeruhiwa
katika ajali ya basi la kampuni ya NBS lenye namba za usajili T 909 BXK
lililo kuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Tabora kuanguka katika eneo
la Tabu Hotel kata ya Chigela wilaya ya Gairo mkoani Morogoro.
Mganga wa hospitali ya wilaya ya Gairo Mushi Mabula amethibitisha
kupokea maiti tano na majeruhi 26 ambapo amesema watu saba hali zao
sinzuri na watahamishiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
Kwa upande wao mashuhuda wakiwemo majeruhi wa ajali hiyo wameeleza
jinsi ajali hiyo ilivyotokea huku mashuhuda wakiwataka madereva
kuzingatia sheria za barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima.
Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya
mkoa wa Morogoro huku majeruhi wakilazwa katika hospitali ya wilaya ya
Gairo.



