Aliyeondolewa Ukuu wa wilaya ajitetea,adai hakubebwa.

Siku moja baada ya Rais John Pombe Magufuli kutangaza upya nafasi za wakuu wapya wa wilaya nchini, aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Lushoto mwenye umri mdogo kuliko wenzake ambaye jina lake limeondolewa katika orodha hiyo Mariam Juma,amedai kuwa nafasi aliyokuwa ameipata sio kwamba alichaguliwa kwa upendeleo,na badala yake elimu ndio iliyosababisha kupata hadhi ya kumuwakilisha Rais wa awamu ya nne.
 
Amezungumza hayo na wazazi,viongozi wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,pamoja na viongozi wa serikali ngazi ya wilaya katika harambee ya kuchangia maendeleo katika chuo cha mafunzo ya ujasiriamali kilichopo vuga wilayani Lushoto.

Awali akielezea shughuli zinazofanywa katika Chuo maalum cha kujifunza ujasiriamali ikiwemo kutengeneza mizinga ya nyuki kwa kutumia udongo wa mfanyanzi,elimu ya mazingira pamoja na kilimo cha mboga mboga ili kuwapunguzia vijana changamoto za maisha,Mkuu wa chuo hicho Mchungaji Yohana Mmaka amesema elimu ya ujasiriamali imekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwawezesha vijana kujitambua.

Kufuatia hatua hiyo,diwani wa kata ya Vuga wilayani Lushoto Jumaa Dhahabu,ameiomba serikali kuu kuwahisha mafungu ya fedha za shughuli za maendeleo katika halmashauri ya wilaya hiyo,kufuatia miradi tofauti ikiwemo ujenzi wa maabara iliyoanzishwa na rais wa awamu ya nne kusitishwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo