WAZIRI Nape ateua

Na Chalila Kibuda, Globu  ya Jamii.
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amewateua wajumbe wanne wa kamati ya maudhui watakaotumikia kipindi cha miaka mitatu.

Taarifa iliyotolewa  leo kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari Maelezo ilieleza kuwa uteuzi huo hufanyika kila baada ya miaka mitatu.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni  Joseph Mapunda ambaye ni  mhariri Mtendaji Mstaafu wa Magazeti ya Serikali(TSN) na  Mkurugenzi Mstaafu wa Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) Abdul Ngalawa.

Wengine ni  Mwandishi wa habari ,Mhadhiri Derek Murusuri  pamoja na Mwandishi wa habari ,Mwanasheria , Zainabu Mwatawala.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo