Makete Kazi imeanza, Watendaji wote wa kata na vijiji waitwa Makao Makuu

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Makete Bw. Francis Namaumbo akifafanua jambo 

Watendaji wa kata na vijiji wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kutenda majukumu yao vizuri kama sheria zinavyowataka ili kuepusha migogoro na matatizo yanayoweza kutokea pindi wanapokiuka sheria hizo

Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na kutoa risiti za malipo wanayoyafanya katika kata ama vijiji vyao pamoja na kusoma mapato na matumizi kwa wananchi wao

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Makete Bw. Francis Namaumbo katika kikao maalum kilichowakutanisha kwa pamoja watendaji wote wa vijiji na kata wilayani Makete kwa lengo la kukumbushana mambo mbalimbali wanayotakiwa kuzingatia katika kutekeleza majukumu yao
 Afisa utumishi wa wilaya ya Makete Bw. Nicodemus Tindwa

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa amesema pamoja na watendaji hao kutakiwa kufanya kazi zao kwa kufuata sheria na taratibu za kazi, lakini atasimamia haki zao kama wafanyakazi pamoja na kusimamia mazingira mazuri ya watendaji hao kutekeleza majukumu yao vizuri bila vikwazo mbalimbali

 

Aidha katika kikao hicho watendaji hao wamepata nafasi ya kuzungumzia changamoto zinazowakabili katika utendaji wao wa kazi ikiwemo na wao kujengewa nyumba za kuishi kama zinavyojengwa kwa watumishi wengine katika maeneo yao


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo