Kama ulinunua Tiketi kuona Mechi a Chad na "Taifa Staaz" soma hii

Baada ya jana Jumapili kutolewa kwa taarifa ya kutokuwapo kwa mchezo wa kutafuta nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa la Afrika, kati ya Tanzania na Chad baada ya Shirikisho la Soka la Chad kutuma barua ya kujitoa katika mashindano hayo, TFF imetoa taarifa kuhusu waliokuwa wamenunua tiketi za mchezo huo ulikuwa ufanyike leo Jumatatu.
Kupitia akaunti ya twitter ya Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametoa taarifa kuwa waliokuwa wamenunua tiketi watarudishiwa pesa zao kuanzia kesho katika vituo ambavyo walinunulia tiketi.
Malinzi aliandika “Kufuatia mechi ya Chad kutokufanyika utaratibu unafanyika ili kesho watazamaji walionunua tiketi warudishiwe fedha zao.”
Tweet nyingine Rais huyo wa TFF aliandika “Watazamaji walionunua tiketi za mechi ya Chad watarudishiwa fedha zao kesho kwenye vituo walikonunulia tiketi jana.Waje na tiketi hizo.”


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo